Open top menu

Muigizaji nyota wa tamthilia ya Isidingo lesego Motsepe afariki

Muigizaji nyota, Lesego Motsepe, ambae alikuwa akijulikana kama Letti Matabanne katika tamthilia ya Isidingo amefariki dunia.
statement iliyotolewa kwa niaba ya familia ya Motsepe inasema kuwa, alikutwa akiwa ameshafariki na kaka yake "Moemise Motsepe" akiwa nyumbani kwake mida ya saa tano asubuhi,

Mwaka 2011, siku ya ukimwi duniani, Motsepe alijitangaza hadharani hali yake ya VVU katika kusaidia kupambana na unyanyappaa dhidi ya watu wanaoishi na ugonjwa huo. Alifanya pia warsha kadhaa na mazungumzo juu ya umuhimu wa kuishi kwa matumaini  kwa walioathirika na Ukimwi moja kwa moja au vinginevyo. Yeye pia alifanya kazi kama balozi wa Ukimwi kwa miaka mingi, kuwaelimisha watoto katika jamii mbalimbali.
Lesego ameelezewa kama binti mwenye upendo, dada na rafiki, alikuwa ni mhitimu wa mchezo wa kuigiza, alikuwa ni muigizaji, mshairi,na mtoa hadithi ambaye alitumia zaidi ya miaka 10 katika sehem kubwa ya tamthilia hiyo maarufu. 
Motsepe aliishi na mama yake - Ivy Skhosana na kaka zake wawili  wawili - Andile Skosana na Moemise Motsepe na wapwa mbalimbali, wajukuu, familia yake ya kiroho na familia pana.

0 comments